Deuteronomy 18:9-14

9 aWakati mtakapoingia katika nchi ambayo Bwana Mwenyezi Mungu wenu anawapa, msijifunze kuiga njia za machukizo za mataifa ya huko. 10 bAsionekane mtu yeyote miongoni mwenu ampitishaye mwanawe au binti yake katika moto, atakayefanya uaguzi, ulozi, anayetabiri nyakati, anayejishughulisha na uchawi, 11 cwala arogaye kwa kupiga mafundo, wala mwaguzi au anayeabudu mizimu, wala awaombaye wafu. 12 dMtu yeyote afanyaye mambo haya ni chukizo kwa Bwana, tena ni kwa sababu ya matendo haya ya kuchukiza wayafanyayo ndiyo maana Bwana Mwenyezi Mungu wenu atayafukuza mataifa hayo mbele yenu. 13 eKamwe msilaumiwe mbele za Bwana Mwenyezi Mungu wenu.

Nabii

14 fMataifa mtakayowafukuza husikiliza wale wafanyao ulozi na uaguzi. Lakini kwenu ninyi, Bwana Mwenyezi Mungu wenu hajawaruhusu kufanya hivyo.
Copyright information for SwhKC